KASUKU MNENAJI
Shairi la ki-leo
KASUKU MNENAJI
Shairi la ki-leo

Mimi ni kasuku mnenaji niliyefungiwa kwenye banda la dhahabu,
maneno yangu matamu nikiwa ndani, mbawa zangu zameremeta
Nikiamka asubuhi nawadhiaki walio nje, na kuwaona hawafai
Kasuku mwenye mikogo, lakini nimefungwa yangu miliki mdomo
Angali mbawa zangu zikiwa ndogo, nilketi nao nje
Tulinena makuu, mabadiliko ya nchi
Fikra zangu silaha, zapotelea kwenye banda la dhahabu
nimekuwa kibogoyo, nikiogopa patilizwa na wenye meno
Sasa nipo ndani wananipitishia vitamu, ila kero yangu matusi
Banda langu la thamani, hata kinyaa sikioni
Wao waniita mfungwa, ni wivu wananionea
Shaba hawana, dhahabu yangu dhihaka
Wanitazamapo hudhuni uwajia, mwenyewe sina habari najionea fahari
Uzio wangu wasafishwa kila siku, macho yajaa ukungu
Sioni ya kwao, wanayaona ya kwangu
Banda langu la thamani, lasimamisha fikra zangu
https://twitter.com/MyHadithi/status/1585936939273723905/video/1
메타데이터
- post_id
- 72a249dd78fc
- slug
- kasuku-mnenaji-72a249dd78fc
- url
- https://medium.com/@msafir/kasuku-mnenaji-72a249dd78fc
- canonical_url
- https://medium.com/@msafir/kasuku-mnenaji-72a249dd78fc
- author_url
- https://medium.com/@msafir
- status
- ok
- fetched_at
- 2026-07-24 14:22:46